Posts

Showing posts from May, 2018

SURA NZURI KUMSOMEA MTOTO WAKO

Image
sura zote 114 za Quran zina faida katika kinga na tiba za maradhi mbalimbali na majanga ya kidunia na akhera, ila zifuatazo ni sura zinazotumika kumsomea mtoto kwa maslahi yake ya sasa na baadae Na Dr. Hamy ~surat Fatiha, hii ni sura ya ufunguzi katika kisomo chako na kitaalam inatibu kila ugonjwa. msomee mtoto mara saba ~ayat kusiy na aya nne za mwisho za surat baqara. aya hizi ni ulinzi mkubwa sana kwa familia yako ~surat ibrahim, imeelezwa kuwa mtoto atakayesomewa sura hii allah atamuepushia maradhi katika umri wake wote. ~surat bani israil, faida ya sura hii ni kwa mtoto anayechelewa kusema. chukua maji uyasomee sura hii kwa yakini halafu mpe anywe ataongea ~surat yaasin imeelezwa kuwa hii ndio moyo wa qur'an, nani utimilifu wa haja. soma sura hii kuipa uzito dua yako ~surat jaathiyah, sura hii akisomewa mtoto mchanga atapata ulinzi dhidi ya kila majanga ~surat tur mtoto atakuwa na afya nzuri ~surat balad ni kinga ya maradhi ~surat nas itamlinda mtoto dhidi ya maji...

FAIDA YA SURA HIZI TATU

Image
1. aya ya 23 ya sura hii ni tiba kwa maradhi ya macho 2. aya ya 37 ni tiba ya maradhi ya moyo 3. msomaji wa sura hii rizki yake huongezeka 4. hakuna mateso wakati wa kifo cha msomaji wa sura hii SURATUDH DHARIYAAT 1. ukichukua maji ukayasomea sura hii na kumpa mgonjwa wa maumivu ya mgongo, atapoa kwa uwezo wa mwenyezi mungu 2. kwa mama mjamzito akisomewa sura hii hujifungua kwa urahisi hata kama uzazi wake ni wa matatizo 3. kifo cha msomaji wa sura hii si cha mateso SURATUT TUR 1. kama sura hii itasomwa kwa ajili ya mtoto mchanga, mtoto huyo atakuwa na afya nzuri 2. kama mtumwa, mateka au mfungwa atasoma sura hii, au jamaa zake watasoma kwajili yake kwa idhini ya allah ataachiwa huru. amini mungu hashindwi na lolote kama una magumu yanayokushinda njoo tumuombe mungu pamoja atusaidie

NI UWEZO GANI ALIONAO MGANGA KUJUA KILA KITU?

Image
MGANGA NI NANI? Mganga ni mtu yeyote mwenye uwezo wa kutibu matatizo ya mwili na akili yanayomsibu mwanadamu mwenzake. Inawezekana ukawa na tafsiri nyingine nzuri kuliko hii yq kwangu lakini hii sio point yangu ya msingi, la msingi ni hili linalofata. JE MGANGA ANAWEZAJE KUJUA KILA AINA YA TATIZO? Uganga ni elimu kama zilivyo elimu zingine hivyo basi huwezi kujua kila kitu na hiyo ni sababu mganga anapaswa kuendelea kujifunza taaluma yake ya Uganda kilq siku ili ajue mambo mengi zaidi. Ni jambo la ajabu sana kukutana na mtu anayejua kila kitu, kuna waganga wao hawatofautiani sana na aliyewaumba kwa maana wao wanajua kila kitu. Hata hivyo hupaswi kuridhika iwapo dawa fulani huijui bali unapaswa kutafuta wataalamu wanaoijua dawa hiyo na kwenda kujifunza hata ikibidi kutoa gharama kubwa kiasi gani almuhimu uijue dawa hiyo ili usihangaike tena akitokea mgonjwa mwingine wa namna hiyo. Jambo baya na la kusikitisha ni pale mtu anapokufata mganga wewe na kukulalamikia juu ya matatizo yak...

TIBA ASILI YA U.T.I

Image
Leo nimependa niwape faida moja ya tiba ambayo itawasaidia mpaka kufa, naamini kila mmoja atapenda somo hili. Chukua ukwaju na tangawizi. Hakikisha ukwaju unaochukua ni ule wa tunda ambazo ni chachu ukila ambazo hutumika kutengeneza juisi. Pia chukua tangawizi ile mbichi kabisa ya kuweka kwenye chai. Saga tangawizi kisha weka kwenye sufuria yenye maji lita moja na nusu, weka na ukwaju humo uanze kuchemsha hadi ichemke sawasawa. Ukwaju utajivua na dawa yako itachanganyika vizuri kwenye maji. Tumia mwiko kukoroga vizuri na kisha uchuje. Tumia dawa hii kwa kunywa kutwa mara tatu kwa siku tatu, ikiisha chemsha tena nyingine utumie kwa siku tatu zingine. Jumla utakuwa umetumia dawa hiyo kwa siku sita. Inshallah wiki ijayo nitakuwa Dodoma, Mbeya na Iringa kwa ajili ya wanaohitaji tiba zangu. Nijuze mapema kama utahitaji tuonane kupitia namba hii 0678659525 Dawa hiyo hapo juu ni dawa kiboko naya uhakika kutibu tatizo la UTI (Urinary Tract Infection).

TIBA ASILI YA KUPATA UJAUZITO

Image
Habari yako mwanandoa! Iwapo umedumu katika ndoa yako kwa mwaka mzima au zaidi hali ya kuwa burudani ya ule mchezo unacheza kama kawaida basi jua wewe una tatizo unastahili tiba. NANI MWENYE TATIZO KATI YENU? Mwanaume na mwanamke wote wanawajibu wa kujiuliza kwanini hawapati mtoto. Mwanaume matatizo yake yanaweza kuwa ni Kutoa mbegu (sperm) zilizokufa Kutoa kiwango kidogo sana cha mbegu (sperm) Udhaifu wa nguvu za kufanya mapenzi na hujikuta akishindwa kushuhurika siku husika ya mimba Wakati kwa mwanamke matatizo yake ni Kukoma uzalishaji wa mayai ya uzazi (Tatizo hili halitibiki) Uzalishaji hafifu wa mayai ya uzazi (kwa kikubwa hii husababishwa na vizuia mimba) Kuziba kwa mirija ya mimba Uvimbe katika kizazi Kutokuzalishwa kwa ute mwepesi katika njia ya kizazi ya mwanamke. Ute katika njia ya kizazi una kazi ya kulainisha njia na kufanya mbegu za kiume ziweze kusafiri vizuri mpaka kufikia mayai ya kike. Mbegu hazitaki kukutana na mchubuko wowote njiani hivyo basi kunapo ko...

DAWA YA KUONDOA WEUSI KATIKA UKE WAKO

Image
KWA WANAWAKE TU ®+18 Habari za wakati huu kwa wapendwa warembo wa kila rangi. Leo nakuletea hii faida ya dawa nzuri kabisa itakayokufaa VIFAA Asali (vijiko 2) Machicha ya nazi (Vijiko 2) Sukari (Vijiko 2) Maji ya ndimu (kijiko 1) UANDAAJI Saga sukari yako au itwange katika kinu (kiuri) hadi ilainike na kuwa unga. Baada ya hapo changanya na vitu hivyo pamoja, ikoroge vizuri ichanganyike MATUMIZI Kwanza nyoa nywele zote katika sehemu za siri uwe safi kabisa. Tumia dawa hii kusugulia katika kona zote za uke wako. Juu na chini, kulia na kushoto. Dr. Hamy  06 78659525 Dawa hii ni dawa nzuri sana ya kuondoa weusi katika uke wako, kuweka ulaini na kuondoa ukavu katika uke wako. Hii ni scrub nzuri sana kwa wadada wanaopenda kwenda na wakati.

FAIDA ZA KINGA

Image
Wengi wetu wamekuwa wakithamini sana dawa lakini kinga hawazithamini abadan. Wakati wa kuumwa pekee ndio mtu anapomtafuta daktari lakini akishapona hakumbuki tena kama kuna mtu muhimu anayeitwa daktari, hii iwe hospitalini au kwa mganga Zipo kinga za namna nyingi ila leo nitazungumzia kinga za mwili na nyumba. Kinga ndio kitu pekee kitakachokufany a usirudirudi kwa mtaalamu kufata tiba kila kukicha. Iwapo unakumbwa na matatizo ya mara kwa mara ukitibiwa leo unqkuwa sawa kabisa lakini baada ya muda tu tatizo linarudia basi ujue wewe unaishi na pamoja na ubaya, hivyo ukiwa na kinga mbaya wako hataweza tena kukuingilia na kukudhuru. Kuna nyumba kila siku wakazi wake hawalali, mara wameingiliwa na wachawi, mara ndoto za ajabu ajabu, mara watoto kulialia n.k Hayo yote yanakomeshwa na kuweka kinga katika nyumba yako. Je wezi wamekuwa adui wa mazao yako shambani? Kila ukilima wanavuna wao. Dawa pekee ya kuwadhibiti wezi ni kuweka kinga. KINGA NI BORA KULIKO TIBA 0678659525

JE SARATANI (CANCER) INATIBIKA?

Image
<fg=b00000ff> najua kila mtu atajibu hapana kwakuwa hajawahi kuona dawa yenye kutibu tatizo hilo, lakini leo nitakufundisha dawa hii ukaitumie mwenyewe halafu utaleta majibu kama Ile kauli ni kweli au hapana inayosema "kila ugonjwa unayo dawa yake isipokuwa uzee na kifo. Kwanza fahamu aina tofauti za saratani kulingana na mahali ilipokutokea. kansa ya tumbo kansa ya kizazi kansa ya kidonda kisichopona kansa ya matiti <fg=b0bf00ff> iwapo kansa imekaa tumboni unatakiwa upate mizizi ya miti mitatu. Ukishapata miti hiyo unatakiwa uitwange unga Kisha changanya unga huo na unga wa mtama. Pika uji mwingi uwe unakunywa hadi kushiba, tumia uji huo kunywa kila siku kutwa Mara tatu kwa muda wa miezi 6. <fg=b0bf00ff> Kwa kansa ya kidonda unatakiwa upate tende mrututu msigi mnuka nyama Funga dawa hizo hatua kwa hatua. Na ufunge kwa kutumia jani la mboga, pamba juu yake na bendeji ni matapa ya ng'ombe wa kiume <fg=f0f00f0f> ONYO: WAKATI WOTE WA TIBA US...

PETE ZA BAHATI 2

Image
Pete zina mambo mengi sana, ukiitazama pete hii haina kito cha rangi yoyote kama Vito tulivyovizoea Lakini hii nayo ni Pete ya bahati. Pete hii katika kichwa utaona ni madini tu ya aina sawa na pete yenyewe lakini ukweli ni kwamba ndani humo kunaingia pesa ya zamani, kunaingia tarasimu maalum kwajili ya mvuto na bahati ambayo makazi yake maalum ni kwenye pete, kitu cha tatu kuingia katika Pete hii ni dawa za miti Ama za kiarabu zote zinachanganywa pamoja na kufunikwa vizuri na madini ya fedha ama dhahabu. Kisha bwana sonara anaitengeneza vizuri Pete hiyo kwa umbo la duara, kopa, kisu 'n.k ili kuwa yenye kupendeza zaidi ivaliwapo. Wengi wetu bado hawajajua nini faida ya pete lakini kwa yoyote anayejua siri hii iliyopo katika Pete hawezi kukosa kuvaa. Hebu watazame waganga, watabiri, na viongozi wa dini. Hawakosi Pete maalum vidoleni mwao. Watazame tena watu maarufu, wasanii, maraisi, wafalme, matajiri wakubwa na mawaziri. Hawakosi pete vidoleni mwao. Inakuwaje wewe ukose kwani...

Kama unampenda mtu hataki hata kukuona, fanya njia hii

Image
Nenda katika mti wa mbaazi siku ya jamaa tano saa moja asubuhi. Ukifika piga hodi Mara tatu, mwagia mtama kidogo, mchele na bisi. Ongea na mti huo ukiuomba jambo ulilolikusudia. Kisha ng'oa mzizi mmoja wa upande linapozama jua uondoke nao. Chukua mchanga wa mguu wa kushoto wa huyo mwanamke unayempenda naww chukua mchanga wa mguu wako wa kulia. Kisha rudi sasa sehemu ya kufanya kazi yako. Tafadhali muda uwe ni saa moja jumaatano kama imeshapita basi subiri mpaka saa nane. Tandika kitambaa cheupe, weka kitu kimoja kimoja huku unakinuwia kumuita huyo umpendae katika mapenzi yako. Ukimaliza vifunge pamoja kwa kutumia uzi mweupe. Ifukize ubani mashtaka, ubani mweupe, uvumba na udi. Ukimaliza nenda kaifukie katika jiko la kuni chini. Huyo mtu atakupenda kuliko kawaida. Dr. Hamy 0678659525

Dawa ya kuvuta wateja katika biashara yako

Image
leo nakufundisha njia rahisi kabisa kuliko zote ambayo pia niya uhakika katika kuvuta wateja katika biashara yako. Kwanza kabisa upate miski halisi kabisa, chukua njiwa mweupe umchinje na damu yake uichanganye na hiyo miski. Tumia hiyo kama wino uandikie maandishi unayoyaona katika picha hii hapa chini. Chukua karatasi hiyo uifunge pamoja na mchanga wa sokoni, mchanga wa stendi, na ubani dhukra. Michanga hiyo unatakiwa uichote wakati kuna watu wengi ili kuvuta watu wengi waje katika biashara yako kama wanavyokuja stendi na sokoni. Kaa chini uanze kuisomea wasilatu shafii Mara tatu kwa saa ya zuhra. Kisha itundike katika biashara yako. Hakikisha unakuwa na wauzaji makini biasharani kwako la sivyo wataona unawatesa bure kwa kutokupumzika. Kwa dawa zingine za biashara na mambo mbalimbali ya kimaisha usisite kunipigia 0678659525

Kinga ya nyumba na shamba ili mchawi asilione

Image
Kinga ya mchawi asione nyumba yako au shamba Kuna siku nilitoa maelezo ya namna ya kutengeneza kinga ya nyumba yako pamoja na shamba lakini wengi wameshindwa wakisema ni njia ngumu, leo nataka niwape njia nyingine Vifaa: Kitoto cha panya ambacho hakijaanza kuona. Kitoto cha ndege wa aina yeyote ambacho hakijaanza kuona. Fimbo ya kipofu. Mzizi wa mbarika ulioota juu ya kaburi. Mzizi wa tulla ulioota juu ya kaburi. Kiazi cha mlangamia. ngozi ya kondoo mweusi. Mzizi wa mbaazi uliomaliza mwaka au zaidi. Namna ya kuandaa dawa Ukishapata vifaa hivyo vyote unatakiwa uanze kupika dawa yako hiyo usiku wa manane tena uhakikishe ni usiku wenye giza hakuna hata mbalamwezi inayowamulika. Tafuta mwenzako wa kupika nae dawa, chukua chungu cha ukubwa wa kutosha kupikia dawa zote hizo. Tafuta pia na kuni za kupikia. Kisha anaekarangiza pishi hilo hatakiwi kuona hivyo afungwe kitambaa cheusi machoni, huku mwingine ambaye anaona ndio atakuwa anamuelekeza na kuchochea kuni. Pia hakikisheni w...

Ndoa za watu na Majini

Image
WAJUE WANAWAKE WALIOOLEWA NA MAJINNI. WAJUE WANAUME WALIOOA MAJINNI. ZIJUE TIBA ZA KISUNA ZA KUONDOSHA TATIZO LA MAJINNI HAO. ZIJUE DUA ZA KUWAFUKUZA MAJINNI HAO. dr. Hamy 0678659525 °°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°° Tatizo hili linawakuta watu wengi sana katika jamii zetu hadi kuwapelekea kuishi kwa unyonge na huzuni baada ya kukosa na kupoteza Yale yaliyokua ni mzuri kwao. Kwamfano wapo waliokuwa na tatizo hili na likawafanya wakose hisia za makutano ya kimwili na wenza wao, ni kwakua wamesibiwa na kuolewa na Majinni au kuoa Majinni. Pia wapo ambao hawajapata bahati ya kuolewa, lakini wanatamani kuolewa. Tatizo anajikuta kaishaolewa na dume la kijinni, hivyo kumfanya asiweze kuolewa na...

JINSI YA KUTENDENEZA NYOKA WA ULINZI

Image
Watu wengi wamekuwa wakizungumzia juu ya kufuga nyoka na watu wengi kwenda kutembelea kama vivutio. Mbali na hao inasemekana kuna watu wanatembea na kamba mifukoni mwao lakini akikurushia tu kamba hiyo inabadilika na kuwa nyoka. Je hii ni kweli? Naam ni kweli NYOKA wanaweza kutumika kwa kazi mbalimbali ikiwemo za ulinzi wa shamba au nyumba n.k Leo nawaletea namna ya kutengeneza nyoka wa kulinda nyumba au shamba lako ila utajua wewe namna ya kujilinda asikudhuru 0678659525 Dr. Hamy Kwanza kabisa chukua majani ya mnazi mweupe na uyaandike majina yote ya barhatiy. Kisha somea kila jani moja surat qamar x3 Ukiisha maliza yaweke majani hayo katika ungo na uweke unga wa mahindi katika ungo huo, kama chakula chao ili wasiwe wakali sana ukienda kuwachukua. Waache hadi kesho yake asubuhi ndipo uende kuangalia na utawakuta wamekuwa nyoka kamili (kuwa makini wasikudhuru maana wanakuwaga wakali sana) Ongea nao uwasihi wabadilike wawe majani. Watabadilika na uwachukue hadi katika shamba au ...

FUNGA NDOA KUPITIA NYOTA 1

Image
Iwapo jibu ni ndio basi fatilia makala hii ya leo nikufundishe njia rahisi ya kutumia nyota ila kumpata mwenzako wa maisha. NYOTA YA MASHUKE NA SAMAKI Hawa wawili ni wapenzi wazuri wakutanapo. Iwapo ww una nyota hiyo ukitaka ndoa chagua mpenzi asiyesoma ni bora zaid kwako kuliko aliyesoma. Utampata tarehe 30 ya mwezi wowote na mtakutana hospitali au hotelini au baada ya ajali. Kuwa maridadi, vaa viatu virefu vya visigino na mlio. Usikose senti kidogo, na usionyeshe kulia au kukata tamaa na kumuhudumia katika ugonjwa wake au jamaa wake wa kike. Kutaneni siku ya alhamis NYOTA YA SIMBA NA NDOO Mpenzi anapenda kukandwa na halendi kutolewa ukali na mtembee kwa haraka, saa za mapumziko ziwe ni saa moja au tano. Uwe muhongaji na ukae karibu na nyumba ya kona. Mwanamke avae kofia au ushungi, na kiuno akibane kwa mkanda, mshipi au kanga. Tendo la ndoa liwe fupi na la kurudiarudia, lakini penda romance na massage. Kutana nae siku ya jumapili. NYOTA YA PUNDA NA MIZANI mpate mpenzi siku ya ...

FUNGA NDOA KUPITIA NYOTA 2

Image
____________________Dr. Hamy NYOTA YA NG'OMBE NA NGE Kutana nae siku ya jumanne saa mbili au saa nane mchana na uwe peke yako, vaa nguo za rangi ya kijani. Mpe chakula cha mafuta mafuta na rojorojo. Usimtazame usoni, mguseguse shingo na mapaja, penda kuimbaimba au vaa haedphone. Mkutanishe na ndugu au rafiki zako. Katika tendo la ndoa inabidi liwe refu na la kurudia rudia. NYOTA YA MAPACHA NA MSHALE Penda sana kuzungumza kiingereza au kusoma soma na kushika gazeti unapotembea mbele yake. Kutana nae siku ya jumatano saa tisa na umpende ndugu yake wa pili. Penda kutafuna tafuna bigG, na zungumza utani kwa wingi huku ukizungumza upesi upesi. Vaa nguo za kitoto, fupi na usikose mkanda. NYOTA YA KAA NA MBUZI Penda sana kununa usicheke ovyo, mpe vitu baridi kama ice cream, pipi, na vitu vya kunyonya. Mvamie na umshike shike kitovu pia umfinyefinye vidole. Tembea nae taratibu na uzungumze nae kwa upole, penda sana mambo yake. Vaa nguo ya bluu isiyoiva. Ishi nae nyumba ya bondeni...

TIBA YA MACHO

Image
DAWA YA MACHO IKIWA YANAUMA chukua mrututu na majani ya mfudu , tia katika makaa ya moto umfushe mgonjwa usoni asubuhi na jioni kwa muda wa siku tatu atapona inshallah DAWA YA MACHO IKIWA HAYAONI MBALI iwe kwa kuathiriwa na kutazama screen kwa muda mrefu, mionzi ya , Computer n.k Ama matatizo mengine yote ya macho . Nenda katika mti uitwao mwinukanguu, chimba upate kiazi chake. Kisafishe bila kutumia maji (kikwangue kwa kisu hadi kiwe Safi kabisa, ondoa udongo wote na ganda la nje) Kitwange katika kinu. Weka maji kidogo na uyatumie maji hayo kudondoshea katika macho yote mawili kila ifikapo muda wa kulala , kwa siku tatu hadi wiki moja tu, utakuwa umepona kabisa

JINSI YA KUMTOA JINI MAIMUNA

Image
Jini Maimuna ni jini linalohusika na habari za mapenzi, na mahusiano. Japo jini hili linaweza kutumiwa na waganga katika kuwapa habari mbalimbali lakini pia anaweza kutumiwa kuja kukuta wewe kilazima umpende mtu au umchukue. Kuna habari nyingi kuhusu jini huyu na matumizi yake mazuri na mabaya wanayafahamu waganga na wachawi  lakini leo hii mimi nitakupa njia za kumtoa iwapo amekukumba mwilini mwako. Kwanza andika sura hizi tatu katika karatasi safi isiyo na mistari kwa kutumia wino wa zafarani ▶surat jinn_ ilaa shatwata ▶surat yasiin_ ilaa mubin ▶ayat qursiy_ yote Baada ya kuandika aya hizo katika karatasi, weka karatasi hiyo katika jagi la maji safi mpaka maandishi yote yatoke katika karatasi. Chukua maji hayo Changanya na kungumanga, mdalasini na marashi rozi. Tumia maji hayo kwa kunywa kila siku kwa muda wa wiki moja jini huyo atakuwa ametoweka kabisa katika mwili na maisha yako kwa ujumla. Zingatia: Wakati wote wa tiba usifanye mapenzi siku za Jumat...

KUTAPISHA UCHAWI TUMBONI

Image
Iwapo unasumbuliwa na vitu vya kichawi tumboni leo nakuletea njia rahisi kabisa ya kuvitoa ukawa salama kabisa. Kwanza utajijuaje kama umelishwa vitu vya kichawi? Kuna dalili mbalimbali za kukutambulisha kuwa umelishwa uchawi. Iwe dawa za kukuroga au vyakula vya wachawi kama nyama za watu, damu za watu n.k Dalili kuu ya kwanza ni kuota unakula. Hii ndoto watu wengi wanaota ila wanapuuzia wakidhani ni ndoto ya kawaida tu. Unaweza kuota unakula vitu vizuri au hata vibaya lakini yote maana yake ni moja tu (unalishwa vitu vya kichawi). Dalili ya pili ni baada ya vitu hivyo kuanza kukuathiri ni kuumwa mara kwa mara hasa maumivu ya tumbo, na hata shida katika kizazi. Maumivu ya tumbo ni dalili kubwa sana kwa mtu aliyelishwa vitu vya kichawi na kupona kwake ni mpaka utolewe vitu hivyo. Dalili ya mwisho ni mambo yako kukwama, kila mpango unaoupanga haufanikiwi basi jua hapo uchawi umeshakithiri katika mwili wako na umeshaota mizizi. Sasa tuangalie tiba yake. Uchawi ulioko tumboni unato...

Kuongeza na kupunguza ute ute ukeni

Image
Habari wapendwa. Leo nawaletea faida za kipekee kabisa. Iwapo mwanamke unasumbuliwa na tatizo la kukosa ute ute katika uke wako, tumia njia hii rahisi kabisa. ▶chukua bamia. Bamia ni lile litumikalo kupikia mboga hususani mlenda au hata kwenye mchuzi ili kupata utelezi. Chukua bamia zako uzikatekate katika vipande vidogo vidogo kisha uviloweke katika maji safi kwa siku nzima. Matumizi. Tumia maji hayo kwa kunywa kila siku kwa muda wa siku 21. Hakikisha unaloweka mapya kila siku ili kupata dawa bora na safi. Dawa ya pili ni kwa wanawake wenye majimaji mengi kwenye uke kiasi kwamba inakuwa kero kwa baba nanii akija kufanya yake. Matatizo ni kama jinsia. Aliyepewa hili amenyimwa hili. Wakati unalalamika huna mwingine analalamika imezidi hivyo basi tusidharau tatizo la kila mmoja wetu. ▶ili kutibu tatizo hili  chukua asali na mafuta ya zaituni. Changanya  na uanze kutumia kwa kunywa kijiko kimoja kila siku kutwa mara  mbili. Pia uwe unapakaa asali huko...

Njia rahisi ya kusafisha nyota yako na kukupa mvuto

Image
Iwapo umekuwa wa kuandamwa na matatizo mbalimbali mikosi na unataka kuwa na mvuto kwa watu. Unaweza kujitibu kwa njia hii rahisi kabisa, Chukua dawa iitwayo ubani mweupe ubani dhukra ubani mushtaka na mjafari changanya na uchemshe na maji ya marashi kisha tumia kuogea usiku na asubuhi kwa siku 21 tu utaona mabadiliko makubwa kikubwa usiwe na shetani mwilini mwako dawa hii ni mujaraabu kwa usafi wa nyota. Shetani ama jini hawezi kuondolewa kwa dawa hii hivyo kama tatizo lako linatokana na uwepo wa majini basi inabidi utolewe kwanza

Anza siku yako na Ishi huru

Image
Blog yako ya ISHI HURU sasa ipo tayari kukupa elimu mbalimbali kuhusu afya yako ya mwili na kiroho kupitia tiba zenye asili ya kwetu Tanzania. Pia dua na visomo mbalimbali vitatolewa hapa kwa faida yako mfatiliaji. Hakika kupitia ISHI HURU utajifunza mambo mapya hujawahi kuyajua kabla. Kuwa mfuasi wetu kuanzia leo