Kinga ya nyumba na shamba ili mchawi asilione

Kinga ya mchawi asione nyumba yako au shamba
Kuna siku nilitoa maelezo ya namna ya kutengeneza kinga ya nyumba yako pamoja na shamba lakini wengi wameshindwa wakisema ni njia ngumu, leo nataka niwape njia nyingine
Vifaa:
Kitoto cha panya ambacho hakijaanza kuona.
Kitoto cha ndege wa aina yeyote ambacho hakijaanza kuona.
Fimbo ya kipofu.
Mzizi wa mbarika ulioota juu ya kaburi.
Mzizi wa tulla ulioota juu ya kaburi.
Kiazi cha mlangamia.
ngozi ya kondoo mweusi.
Mzizi wa mbaazi uliomaliza mwaka au zaidi.
Namna ya kuandaa dawa
Ukishapata vifaa hivyo vyote unatakiwa uanze kupika dawa yako hiyo usiku wa manane tena uhakikishe ni usiku wenye giza hakuna hata mbalamwezi inayowamulika.
Tafuta mwenzako wa kupika nae dawa, chukua chungu cha ukubwa wa kutosha kupikia dawa zote hizo. Tafuta pia na kuni za kupikia. Kisha anaekarangiza pishi hilo hatakiwi kuona hivyo afungwe kitambaa cheusi machoni, huku mwingine ambaye anaona ndio atakuwa anamuelekeza na kuchochea kuni.
Pia hakikisheni wote wawili mmevaa kaniki wakati huo wa kupika dawa hiyo.
Dawa ikishaiva tayari utaitoa na kuiweka katika kibuyu au katika kopo jeusi tayari kwa matumizi.
Dawa hii ni miongoni mwa dawa kubwa mno ambazo waganga masharobaro hawawezi kuziandaa.
Dawa hii inamfunga mchawi akija eneo lako haoni kitu pia hata ukiitumia katika mwili wako akikujia kwa lengo la kukudhuru hakuoni.
Pia wezi nao wanaitumia kwenda kuibia wasionekane japo sitafundisha wizi.
Dr.Hamy

Comments

  1. Kwa zaidi ya miaka 13 ya ndoa sikuweza kuzaa, naendelea kuharibika hata nikipata mimba, madaktari wote hawakuweza kunisaidia, hadi dada yangu akanielekeza kwa Dr DAWN, ambaye alinisaidia nikapata ujauzito na sasa hivi kuwa na mtoto mzuri wa kike,
    Anasaidia pia marafiki zangu wengi niliowaelekeza, Dr DAWN ni baraka kwa kila mtu anayewasiliana naye,
    *Kama unataka kupata mimba.
    *Ukitaka kuacha kuharibika kwa mimba.
    *Ukitaka kumrudisha mpenzi wako.
    *Kama unataka mume/mkeo arudishwe.
    *Kama unataka kurejesha mali yako iliyoibiwa au Pesa.
    *Ukitaka kutibu aina yoyote ya ugonjwa,
    Wasiliana naye kwa WhatsApp: +2349046229159

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Njia rahisi ya kusafisha nyota yako na kukupa mvuto

Kama unampenda mtu hataki hata kukuona, fanya njia hii

Dawa ya kuvuta wateja katika biashara yako