JINSI YA KUMTOA JINI MAIMUNA
Jini Maimuna ni jini linalohusika na habari za mapenzi, na mahusiano.
Japo jini hili linaweza kutumiwa na waganga katika kuwapa habari mbalimbali lakini pia anaweza kutumiwa kuja kukuta wewe kilazima umpende mtu au umchukue.
Kuna habari nyingi kuhusu jini huyu na matumizi yake mazuri na mabaya wanayafahamu waganga na wachawi lakini leo hii mimi nitakupa njia za kumtoa iwapo amekukumba mwilini mwako.
Kwanza andika sura hizi tatu katika karatasi safi isiyo na mistari kwa kutumia wino wa zafarani
▶surat jinn_ ilaa shatwata
▶surat yasiin_ ilaa mubin
▶ayat qursiy_ yote
Baada ya kuandika aya hizo katika karatasi, weka karatasi hiyo katika jagi la maji safi mpaka maandishi yote yatoke katika karatasi.
Chukua maji hayo Changanya na kungumanga, mdalasini na marashi rozi.
Tumia maji hayo kwa kunywa kila siku kwa muda wa wiki moja jini huyo atakuwa ametoweka kabisa katika mwili na maisha yako kwa ujumla.
Zingatia: Wakati wote wa tiba usifanye mapenzi siku za Jumatatu, Alhamisi na Jumamosi.
Ukifanya siku hizi utakuwa umeharibu dawa na jini huyo hataweza kutoka.
Kwa tiba zaidi njoo tushirikiane pamoja
Jamn me Batman atoke
ReplyDelete